Thursday, January 18, 2018

WATOTO WENYE SHIDA WAFAIDIKA NA BIMA YA AFYA

 Wageni wa Makao ya Taifa ya Watoto Kurasini wakiangalia moja ya mradi wa ufugaji unaofadhiliwa na na Mfuko wa Abbot Tanzania katika Makao ya Taifa Dar es Salaam  aliye katikati ni Makamu wa Rais wa Mfuko wa Abbot  Bi. Jenna Daugherty.
 Baadhi ya watoto wa Makao ya Taifa ya Watoto wakiimba mbele ya wageni kutoka wafadhili wa Makao yao Abbot Tanzania pamoja na uongozi wa Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto jijini Dar es Salaam.
 Baaadhi ya Maafisa Ustawi wa Jamii kutoka Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto  pamoja na Wafanyakazi wa Makao ya Watoto  wakifuatilia kwa makini maigizo ya Watoto wanalelewa kituoni hapo pichani ni Bi. Ferediana Kiromo kushoto na kulia kwake ni Beatrice Mwatujobe wote kutoka Wazira ya Afya.
Mlezi wa Makao ya Taifa ya Watoto Bi. Beatrice Mugubilo akiongoza wageni wa Makao yake kuangalia maendeleo ya miradi inayofadhiliwa na Mfuko wa Abbot Tanzania.
Na Anthony Ishengoma.

Watoto wanaoishi katika Makao ya Taifa ya Watoto Kurasini wamefaidika na huduma ya Bima ya Afya kwa ajili ya matibabu yao baada ya shirika la Abbot Tanzania kuwezesha ufadhili wa huduma hiyo muhimu pamoja kuwafungulia akaunti za benki ili waweze kumudu kulipia upya wakati bima zao zinapofikia mwisho wa muda wake.

Shirika hili limekuwa mfadhili mkuu wa Makao ya Taifa ya watoto tangu mwaka 2001na limewezasha watoto wa kituo hiki kuhakikisha wanapata huduma mbalimbali ikiwemo ustawi wa watoto kiafya na huduma nyinginezo kama vyeti vya kuzaliwa, ujenzi wa mabweni pamoja na huduma za miundombinu ya kituo hicho.
Makao ya Taifa ya watoto wenye shida Kurasini yametembelewa na ujumbe maalum katoka Shirika linalofadhili kituo hiki la Abbot Tanzania ili kujionea Maendeleo ya shughuli za kituo hicho zinazofadhiliwa na shirika hilo.
Akiongea wakati wa kuwakaribisha wageni hao kituoni hapo, Kaimu  Kamishina wa Ustawi wa Jamii Simon Panga amesema Shirika la Abbot Tanzania limekuwa likitoa ifadhili wake kwa kituo hiki tangu mwaka 2001 na kufanikiwa kuleta mageuzi makubwa kwa Maendeleo ya kituo hiki.
Kamishina Panga ameongeza kuwa pamoja na ufadhili was shirika la Abbot Tanzania, serikali imehakikisha huduma muhimu kama vile chakula, malazi, mavazi, matibabu na elimu vinapatikana kwa watoto wote wanaoishi katika Makao ya Watoto Kulasini.
“Watoto huletwa katika kituo hiki kupitia Maofisa wa Ustawi wa Jamii kutoka Hamashauri zote nchini wakiwa na taarifa zilizokamilika kulingana na mazingira waliyotoka na kuanza maisha kituoni hapa kwa ufadhili wa wasamalia na wafadhili kwa kushirikiana na serikali amesema Kamishina Panga.,”
Historia ya kituo inaanza mwaka 1966 pale Wamissionari walipokianzisha kwa lengo la kulea Watoto yatima. Kituo kilianza na  idadi ya Watoto watatu na baadaye kukabidhiwa rasmi kwa serikali ya Tanzania mwaka 1968 na tangu wakati huo serikali ilibadili mfumo wake na kuanza kutoa huduma ya malezi kwa watoto wote wenye shida.

No comments: