Friday, March 31, 2017

BALOZI WA UINGEREZA NCHINI BI. SARAH COOK AMTEMBELEA KAMISHNA JENERALI WA MAMLAKA YA KUDHIBITI NA KUPAMBANA NA DAWA ZA KULEVYA BW. ROGERS WILLIAM SIYANGA.

Balozi wa Uingereza nchini Tanzania Bi. Sarah Cook Leo amemtembelea ofisini kwake Kamishna Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti na  Kupambana na dawa za kulevya  Bw. Rodgers William Siyanga na kufanya mazungumzo ya  namna serikali za  Uingereza  na Tanzania zitakakavyoweza kushirikiana katika kudhibiti tatizo la dawa za kulevya . Katika ziara hiyo Balozi Cook aliambatana na maafisa kutoka ubalozi wa Uingereza nchini Tanzania  Bw. Christopher Kiddle na Bw. Andrew Stephens.
Balozi wa Uingereza nchini Tanzania Bi. Sarah Cook (wapili kutoka kushoto) alipomtembelea  Kamishna Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti na  Kupambana na dawa za kulevya  Bw. Rodgers William Siyanga (wa kwanza kulia) ofisini kwake leo asubui Jijini Dar es salaam. Balozi Cook aliambatana na maafisa kutoka ubalozi wa Uingereza nchini Tanzania Bw. Christopher Kiddle (wa kwanza kushoto) na Bw. Andrew Stephens (wa tatu kushoto), kutoka kulia (wapili) Makamishna wa Mamlaka ya Kudhibiti na  Kupambana na dawa za kulevya

No comments: