Friday, July 31, 2015

BALOZI DR MAHIGA DAWA SI KUHAMA CCM ASEMA YEYE NI MKOMBOZI WA CCM IRINGA MJINI.

Balozi Dr Mahiga -Iringa mjini.

Na matukiodaimaBlog
ALIYEKUWA balozi wa kudumu  wa umoja  wa mataifa (UN) na mgombea urais katika mchakato  wa ndani ya chama cha mapinduzi (CCM) balozi Dr Augustono Mahiga anayeomba kuteuliwa kuwa mgombea ubunge jimbo la Iringa mjini kupitia CCM amewashangaa makada  maarufu wa chama  hicho  walioshindwa katika mchakato wa ndani ya chama kwa nafasi ya urais kuhama chama hicho kuwa hao hawakuwa na mapenzi ya kuwatumikia  watanzania na kuwa watazunguka kote ila chama makini ni CCM pekee na kuwataka wana CCM jimbo la Iringa mjini kumpa nafasi yeye ili kuondoa masalia ya Chadema .

Balozi Dr Mahiga  alisema kuwa wana CCM hao  walioanza kuhama chama  kwa kukosa nafasi ya urais hawakuwa na mapenzi mema na CCM bali  walikuwa wawametanguliza  maslahi yao mbele na  kuacha kuangalia maslahi ya Taifa na chama hivyo ni vema watanzania  kuwatazama kwa jicho la tatu na ikiwezekana kuwachunguza japo kwa miaka 5 bila kuwachagua kuwa  viongozi  wao.

Alisema kuwa kama  suala ni uongozi kwa ajili ya  kuwatumikia  wananchi na chama kulikuwa hakuna  sababu ya kuhama chama ama kuanza kutukana chama kwa sasa ila wangeweza  kushuka chini na  kugombea nafasi za chini ukiwemo udiwani ama ubunge kama ambavyo  yeye alivyoshuka na kugombea ubunge ili kuwatumikia watanzania kwa ngazi ya ubunge.

"Kila nafasi ndani ya chama ina maana  kubwa katika kutumikia  watu hivyo kuhama chama si jambo jema na upande wa vyama lazima kuwa makini na wanachama wanaohama vyama kwa sasa ili  kupata nafasi za uongozi iwapo  watakosa nafasi hizo  bila shaka  watachukua hatua ya  kuvuruga nguvu ya vyama  hivyo ama kuhama vyama "

Balozi Dr Mahiga  aliyasema hayo  wakati akizungumza na waandishi wa habari mjini Iringa kuhusiana na mchakato mzima wa kumpata mgombea Urais wa CCM Dr  John Magufuli na mchakato wa kura  za maoni  katika ngazi ya udiwani na ubunge katika  jimbo la Iringa mjini ambako  ni mmoja kati ya  wana CCM 14  wanaoomba kuteuliwa kuwa wagombea wa ubunge .


Alisema akiwa kati ya  wana CCM 41 waliojitokeza  kuchukua fomu ya Urais hana kinyongo na uteuzi wa mgombea  Urais wa CCM Dr Magufuli kwani ni mtu  makini na safi ambae  viatu  vya Rais wa awamu ya nne Dr Jakaya Kikwete ataweza  kuvimudu  vema kutokana na kutokuwa  mtu wa kulipisha  kisasi na hana  makuu na mtu  zaidi ya  kulitumikia Taifa  .

Hivyo alisema iwapo wana CCM  jimbo la Iringa mji watamchagua yeye  kuwa mgombea ubunge  jimbo  hilo wawe imani  ya  kulikomboa jimbo hilo asubuhi  saa 12 kutoka kwa  Chadema  chini ya aliyekuwa mbunge  wa jimbo hilo mchungaji Peter Msigwa kwani alisema  si kweli kama Chadema Iringa mjini wananguvu kubwa kuliko  ya CCM na ukitazama idadi ya wenyeviti wa mitaa ambao CCM inao wenyeviti  104  huwezi linganisha na  wale 64 wa  Chadema kabla ya wenyeviti wake 13 kuvuliwa nafasi zao  na mahakama.

Alisema dawa ya ushindi  wa kishindo kwa CCM Iringa mjini ni moja pekee  kuvunja makundi na kuwa kundi moja la ushindi baada ya zoezi la kura za maoni kumalizika .
Dc Mwamoto  kulia akiwa na mbunge wa Kalenga Godfrey Mgimwa ,mwamoto ni mgombea ubunge Kililo

Mkuu wa wilaya  ya Kaliuwa mkoani Tabora Bw  Venance Mwamoto ambae anawania kuteuliwa kuwa mgombea ubunge  jimbo la Kilolo mkoani Iringa amesema kuwa tishio la  kutaka kuuwawa kwake  majuzi baada ya  kufyatuliwa risasi katika gari lake  wakati akitoka katika kampeni  kata ya  Ilula bado haimtishi  katika safari yake ya  kuwatumikia  wananchi  wa jimbo la Kilolo linaloongozwa na Prof. Peter Msolla .

Kwani alisema moja kati ya ahadi yake  kubwa kwa wananchi wa Kilolo ni  kuona amawatumikia kwa kasi zaidi na kumaliza kero ya maji katika mji  wa Ilula na changamoto nyingine ambazo hazijapatiwa ufumbuzi kwa kipindi kilichopita na mbunge  aliyekuwepo .

Mwamoto  alisema kuwa kazi nzuri  aliyoifanya kwa nafasi ya  ukuu  wa wilaya  kwa kipindi  kifupi ambacho  Rais Dr Jakaya kikwete alipomteua kwa  kuwa mkuu  wa wilaya ya  Kibonde na Kaliuwa ni wazi ni  kipimo tosha na heshima kubwa ya wananchi  wa Kilolo kujivunia na  wategemee makubwa zaidi  iwapo  watamchagua kuwa mbunge  wao kwa  sasa .
                                             waziri Lukuvi - Isimani

Mbunge  wa  jimbo la Isimani Bw  Wiliam Lukuvi amewaomba wananchi  wa jimbo  hilo hasa  wanachama wa CCM kuendelea  kujenga imani kwake na kuwa ndani ya CCM kuna Demokrasi  na kila mwanachama ana sifa ya  kugombea nafasi  yoyote ndani ya  chama japo  kipimo  cha kuchaguliwa bado kipo  kwa wananchi  wenyewe ambao  wanaweza kumpima kwa kazi alizofanya badala ya kushawishiwa kwa manenio bila vitendo.

Lukuvi ambae ni waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi amesema kama  si wana Isimani kuonyesha ushirikiano  wao kwake na hata  kumchagua katika nafasi hiyo ya  ubunge basi heshima ambayo  ambayo  wana Iringa wameipata  kupitia  wizara yake leo  isingekuwepo .

Alisema suala la migogoro  ya ardhi  amepata  kulishughulikia kwa umaniki mkubwa na kuwa sulaa  hilo pia  lilikuwa ni kero kubwa hata kwa wananchi wake wa jimbo la Isimani ila kwa sasa kwa kiasi  limeanza kupungua na kuwa iwapo wataonyesha imani yao tena  wategemee kuona maendeleo makubwa zaidi katika jimbo hilo na kutaka baadhi ya kazi kubwa ambazo zimefanyika kuwa ni pamoja na barabara ya lami ya Iringa- Dodoma, umeme  vijini , ujenzi wa shule pamoja na ujenzi wa nyumba bora  kwa kupata bati za ruzuku .

"Tumekuwa pamoja  muda  wote katika maendeleo  na matatizo  hivyo lazima  kila  safari ina  wasindikizaji  wake na siku  zote penye maendeleo ndipo panapopendwa na wengi  ila bado kwa tathimini yetu Ismani ya  leo  sio ya jana . nimekomesha ulanguzi wa mazao kama mpunga ,alizeti  kwa kufunga mashine"
                   Godfrey Mgimwa -Kalenga

Mbunge wa jimbo la Kalenga  Godfrey Mgimwa anayeomba kuteuliwa tena kuwa mgombea wa CCM nafasi ya ubunge  amewashukuru wananchi  wa kalenga kwa kuonyesha ushirikiano kwake na kuwa hadi  sasa amepata  kutekeleza ahadi zake kwa wananchi kwa asilimia 99 na kuwa zipo changamoto mbali mbali ambazo  watampa tena nafasi ya ubunge atakwenda  kuzifanyia kazi .

Mgimwa ambae  amepata  kuongoza jimbo hilo kwa mwaka mmoja pekee akichukua nafasi iliyoachwa wazi na aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo Dr Wiliam Mgimwa aliyefariki duni mwaka jana mwanzioni ,alisema zilikuwepo ahadi mbali mbali ambazo ziliachwa na mbunge aliyepita na tayari zote amezikamilisha kwa kipindi cha mwaka mmoja na kubwa anajivunia kuanzisha vikundi vya Vicoba  zaidi ya 60 ,ujenzi wa barabara , maji  vijiji ,umeme na uchangiaji wa ujenzi wa zahanati ,shule  na maabara na kuwa zaidi ya Tsh milioni 100 amepata  kutumia kwa kuchangia miradi ya maendeleo jimboni.

1 comment:

Anonymous said...

Wewe Mahiga unaweza ukatumikia nchi kwenye chama chochote kile siyo lazima kiwe CCM, Nchi na chama ni vitu viwili tofauti. Waliohama chama wanatekeleza demokrasia na ni haki yao ya msingi kama vile wewe ukivyotafuta opportunity ya kuwa mbunge baada ya kushindwa kwenye urais. Hao wanaohama wanayo akili timamu, wewe kama umeamua kubaki CCM ni uamuzi wako ndiyo maana hakuna anayekuingilia au anayekusema vibaya, hivyo na wewe uache kuwasema vibaya wenzako wanaohama ndiyo maana kuna vyama vingi. Kumbe ungekuwa rais ungekuwa na closed mind.......si lazima kila mtu afanye wewe unavyoona ni sawa au afikiri wewe unavyofikiri. Nategemea utanielewa daktari.