Tuesday, June 30, 2015

ACACIA YAKUSANYA SHILINGI MILIONI 800 ZA KUSAIDIA SEKTA YA ELIMU, BAADA YA KUPANDA MLIMA KILIMANJARO

 MKUU wa wilaya ya Tarime Mkoani Mara, Glorious Luoga, (Katikati), akinyanyua juu mfano wa hundi yenye thamani ya shilingi Milioni 800, baada ya kukabidhiwa na Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampouni ya Acacia, Brad Gordon, (kushoto), katika hafla fupi iliyofanyika kwenye lango la kushukia kutyoka kilele cha  Mlima Kilimanjaro, Mweka, Juni 28, 2015,  Fedha hizo ambazo ni kwa ajili yab kusaidia sekta ya eli kwa watoto kutoka familia duni, zimetokana na wafanyakazi wa Acacia na familia zao pamoja na marafiki, kupanda Mlima Kilimanjaro kwa nia ya kuchangisha fedha chini ya mpango wa kampuni hiyo wa "CanEducate".

Kampuni ya Uchimbaji Acacia, inayojishughulisha na uchimbaji na utafutaji madini, , imekusanya zaidi ya shilingi milioni 800 kupitia upandaji wa hisani wa mlima Kilimanjaro ambao unalenga kuchangisha fedha za kusaidia sekta ya elimu nchini chini ya mpango wa “CanEducate”, uliobuniwa na kampuni hiyo miaka mitano iliyopita.
Timu ya wafanyakazi, marafiki na wanafamilia wa Kampuni ya Acacia wapatao 21 wakiongozwa na Afisa Mtendaji Mkuu, Brad Gordon, wamerudi kutoka safari ya kupanda mlima Kilimanjaro iliyowachukua siku sita.
Kupitia mpango huo wa CanEducate, mpango ambao unatoa ufadhili wa elimu kwa watoto wanaotoka familia duni, zinazoishi maeneo yanayozunguka migodi inayomilikiwa na kampuni hiyo, ya North Mara, Bulyanhulu na Buzwagi, Acacia imeanza utaratibu wa kila mwaka wa kualika wafanyakazi, marafiki na wahisani kuchangisha fedha kwa njia hiyo ya upandaji mlima.
Akizungumza na wandishi wa habari kwenye lango la kushukia la Mweka, Afisa Mtendaji Mkuu wa Acacia amesema ni jambo la kujivunia kuona kampuni imefikia lengo la kukusanya kiwango cha dola 200,000, sawa na shilingi za Kitanzania Milioni 800, kupitia zoezi hili, fedha ambazo zitakuwa na matokeo makubwa sana  kwa kugusa maisha ya watoto wengi nchini Tanzania.
“Tayari tumekwisha fikia lengo la kukusanya dola 200,000 huku michango zaidi ikiendelea kumiminika. Tunayaasa makampuni na watu binafsi kuendelea kuchangia kwani zoezi lipo wazi hadi mwisho wa mwezi Julai,” alisema Brad.
Aidha, ameongeza kuwa kwa kila dola moja itakayochangwa na wafadhili, pia Kampuni ya Acacia itaongeza dola moja na hivyo kufanya jumla ya fedha zitakazoelekezwa kusaidia sekta ya elimu kupitia mpango huu kufikia kiasi cha dola 400,000 kwa mwaka huu.
Kwa kuzingatia kuwa inagharimu kiasi cha dola 75 kwa mwaka kupeleka mwanafunzi shuleni nchini Tanzania, fedha zilizokusanywa zina uwezo wa kusaidia wanafunzi zaidi ya 2,000 wasioweza kumudu gharama za masomo hususani kutokea jamii jirani na migodi ya Acacia yaani Buzwagi, Bulyanhulu na North Mara iliyoko mkoani Shinyanga na Mara.
Mpango wa CanEducate ulianza mwaka 2010 kwa kuwanufaisha wanafunzi takribani 158 katika maeneo ya Bulyanhulu na hadi mwisho wa mwaka 2014 mpango umekuwa hadi kufikia kuwanufaisha wanafunzi zaidi ya 1,800 katika maeneo ya Bulyanhulu, Buzwagi na North Mara na wanafunzi hawa wameonyesha ufaulu mzuri katika shule mbalimbali katika mitihani yao ya Taifa.
Mlima Kilimanjaro,, unatambulika kuwa  mlima mrefu zaidi barani Afrika nan i wa tatu duniani ambao kufikia kilele cha Uhuru mita 5,895 ni hatua ya juu barani Afrika. Kampuni ya Acacia ina mtazamo kuwa  Elimu humfanya binadamu kuwa huru sababu ambayo inaufanya mpango wa CanEducate kufaa kukusanya  fedha kupitia kupanda mlima hadi kufikia kilele cha Uhuru Peak.
Waweza kuchangia Elimu kupitia upandaji mlima huu wa hisani, kupitia tovuti ifuatayo;
http://caneducate.ca/kili-climb.html
 Brad, (kushoto), akikabidhi hundi hiyo kwa Mkuu wa wilaya ya Tarime, Glorious Luoga
 Brad, akizungumza wakati wa kukabidhi hundi hiyo, akiwa
 Brad Gordon, (wakwanza kulia), akiongoza timu ya watu 21, wakiwemo wafanyakazi wa Acacia na familia zao pamoja na marafiki, kushuka Mlima Kilimanjaro wakitokea kileleni, kwenye lango la Mweka
 Furaha baada ya kufanikiwa kufika Kilele cha Mlima Kilimanjaro na kurejea salama
 Afisa Mtendaji Mkuu wa Acacia, Brad  Gordon, (Katikati), Makamu wa Rais wa Acacia anayeshughulikia masuala ya kampuni, Deo Mwanyika, (wakwanza kulia), Meneja Mkuu wa uendelezaji wa kampuni ya Acacia, Asa Mwaipopo, (wapili kulia), Mkuu wa wilaya ya Tarime Glorious Luoga, (watatu kulia),wakiwa katika picha ya pamoja na watu 21 waliofanikiwa kupanda Mlima Kilimanjaro
 Brad, akipongezana na Deo
Deo akitoa shukrani baada ya timu ya watu 21, walioongozwa na Brad, kufanikiwa kupanda na kurejea salama kutoka kilele cha mlima Kilimanjaro

No comments: