Sunday, May 31, 2015

UHAMIAJI YASHIRIKI KATIKA MAONYESHO YA KARIBU TRAVEL MARKET FAIR, JIJINI ARUSHA

Waziri wa Utalii na Mali Asili, Mhe. Lazaro Nyalandu (Mb.) akisikiliza kwa makini maelezo kutoka kwa Afisa Uhamiaji, Rosemarry Mkandala wakati alipotembelea Banda la Idara ya Uhamiaji mara baada ya kufungua rasmi Maonesho ya Utalii “Karibu Travel Market Fair” mnamo tarehe 29.05.2015 yaliyofanyika katika viwanja vya Kisongo nje kidogo ya jiji la Arusha.
Waziri wa Utalii na Mali Asili, Mhe. Lazaro Nyalandu (Mb.) akisaini kitabu cha wageni alipotembelea Banda la Idara ya Uhamiaji tarehe 29.05-2015 na kuipongeza Idara ya Uhamiaji kwa juhudi zake za kuendelea kushiriki kwenye Maonesho ya Utalii “Karibu Travel Market Fair” yaliyofanyika katika viwanja vya Kisongo nje kidogo ya jiji la Arusha ambapo pia alisisitiza umuhimu wa ushirikiano baina ya Taasisi hizo mbili katika kukuza sekta ya Utalii nchini.
Waziri wa Utalii na Mali Asili, Mhe. Lazaro Nyalandu (Mb.) akipokea machapisho mbali mbali yanayolenga kuelimisha jamii taratibu za Utoaji wa Huduma za Uhamiaji nchini, mapambano dhidi ya Uhamiaji Haramu na makosa mengineyo ya Kiuhamiaji, wakati alipotembelea Banda la Idara ya Uhamiaji kwenye Maonesho ya Utalii “Karibu Travel Market Fair” yaliyofanyika katika viwanja vya Kisongo nje kidogo ya jiji la Arusha.
Maafisa wa Uhamiaji wakitoa Elimu juu ya masuala mbali mbali ya Kiuhamiaji nchini kwa wananchi na wadau mbali mbali walipotembelea Banda la Idara ya Uhamiaji wakati wa Maonesho ya Utalii “Karibu Travel Market Fair” yaliyofanyika katika viwanja vya Kisongo nje kidogo ya jiji la Arusha jana.
Afisa Uhusiano wa Idara ya Uhamiaji, Tatu Burhan akizungumza na mgeni alietaka kujua taratibu za kupata vibali vya ukaazi nchini, wakati alipotembelea Banda la Idara ya Uhamiaji jana (30.05.2015) kwenye Maonesho ya Utalii “Karibu Travel Market Fair” yaliyofanyika katika viwanja vya Kisongo nje kidogo ya jiji la Arusha.
Kamishna wa Uhamiaji (Utawala na Fedha), Piniel O. Mgonja, akisaini kitabu cha wageni na kupokea taarifa ya Ushiriki wa Idara kutoka kwa Afisa Uhusiano wa Idara ya Uhamiaji, Tatu Burhan alipotembelea Maonesho ya Utalii “Karibu Travel Market Fair” jana (30.05.2015) yaliyofanyika katika viwanja vya Kisongo nje kidogo ya jiji la Arusha.
Kamishna wa Uhamiaji (Utawala na Fedha), Piniel O. Mgonja, akiwa pamoja na Maafisa Walioshiriki kwenye Maonesho ya Utalii “Karibu Travel Market Fair” yaliyofanyika katika viwanja vya Kisongo nje kidogo ya jiji la Arusha. Kulia kwake ni Afisa Uhamiaji Mkoa wa Arusha, Naibu Kamishna Danson Mwakipesile, akifuatiwa na Naibu Kamishna wa Uhamiaji Vitalis Mlay, kushoto kwake ni Afisa Uhusiano wa Idara ya Uhamiaji Tatu Burhan.

Kamishna wa Uhamiaji (Utawala na Fedha), Piniel O. Mgonja, akitoa ufafanuzi kuhusu masuala mbalimbali ya Uhamiaji wakati akizungumza na vyombo vya habari jana (30.05.2015) walipotembelea Banda la Idara ya Uhamiaji kwenye Maonesho ya Utalii “Karibu Travel Market Fair” yaliyofanyika katika viwanja vya Kisongo nje kidogo ya jiji la Arusha.
Baadhi ya wageni wakichukua machapisho mbali mbali ili kuelewa vyema masuala mbali mbali ya Kiuhamiaji nchini, wakati walipotembelea Banda la Idara ya Uhamiaji kwenye Maonesho ya Utalii “Karibu Travel Market Fair” yaliyofanyika katika viwanja vya Kisongo nje kidogo ya jiji la Arusha jana.

No comments: