Friday, January 31, 2014

SHULE YA MSINGI KABALE BUKOBA VIJIJINI YAPOKEA UGENI WA MRADI WA "OPPORTUNITY EDUCATION FOUNDATION" TOKA MAREKANI

Mwanafunzi wa Shuke hiyo ya Kabale iliyopo Bukoba Vijijini akimkabidhi Bw. J. Joe Ricketts maua ikiwa ni ishara ya kumkaribisha mgeni huyo kutoka USA kupitia Mradi wa (Opportunity Education Foundation) kwenye shule hiyo leo hii.
Bw. J. Joe Ricketts  kutoka USA kupitia Mradi wa (Opportunity Education Foundation)  akiingia kwenye eneo la Shule hiyo kwenye shule hiyo ya Kabale, Baada ya kupokelewa na Walimu wa Shule hiyo. Kutoka kushoto wa Pili ni Mwalimu Mkuu wa shule hiyo Bi. Kalafaelia Madiloba na kulia ni Dada Sandra aliyeambatana nae Mgeni huyo Bw. Joe Ricketts kutoka USA.
Wanafunzi wa Shule Kabale wakimkaribisha Mgeni huyo kwenye Shule yao leo.
Bw. J. Joe Ricketts  kutoka USA kupitia Mradi wa (Opportunity Education Foundation)  akiingia kwenye eneo la Shule hiyo na hapa alikuwa akiteta jambo na  Dada Sadra
Bw. J. Joe Ricketts  kutoka USA kupitia Mradi wa (Opportunity Education Foundation)  akisikiliza wimbo alioandaliwa na Wanafunzi wa Shule hiyo. Mradi huu wa Opportunity Education Foundation umewafadhili  Shule hiyo Vifaa vya kufundishia, na pamoja na swala la Chakula na Uji kuanzia Darasa la kwanza mpaka la Saba.Wanafunzi wa Shule Kabale wakimwimbia  Mgeni huyo Bw. J. Joe Ricketts wimbo uliokuwa na Ujumbe
Baadhi ya Walimu wa Shule hiyo wa pili kutoka kushoto ni Bw. Mohamed Dauda Mkuu wa Shule Msaidizi.
Mkuu wa Shule ya Kabale iliyopo Bukoba Vijijini Bi. Kalafaelia Madiloba
Mkuu wa Shule ya Kabale iliyopo Bukoba Vijijini Bi. Kalafaelia Madiloba (kushoto) akisoma Ujumbe mbele ya Bw. J. Joe Ricketts  kutoka USA kupitia Mradi wa (Opportunity Education Foundation)
Bw. J. Joe Ricketts  kutoka USA kupitia Mradi wa (Opportunity Education Foundation) Kulia akiwa kwenye maongezi na Bw. Mbaki Mutahaba (kushoto) ambaye ni Mkurugenzi wa Opportunity Education Foundation. (O.E.F)
Mkuu wa Shule ya Kabale(kulia) akifurahia jambo kutoka kwa Bw. J. Joe Ricketts  wakati anamtembeza kwenye maeneo ya Shule hiyo ya Kabale.
Bw. J. Joe Ricketts - Benefactor
Bw. J. Joe Ricketts amejionea swala zima la ugawaji uji kwa Wanafunzi wa Shule hiyo ya Kabale na yeye akashiriki zoezi hilo la ugawaji Uji kwa Wanafunzi.
Baadhi ya Wanafunzi wakifurahia hapa baada ya kupata Ugeni huo kutoka USA
Bwana J. Joe Ricketts akikabidhiwa zawadi na Mwalimu wa Shule hiyo ya Kabale leo
Picha ya Pamoja ya Walimu wa Shule ya Msingi Kabale iliyopo Bukoba Vijijini. Picha zote na Faustine Ruta

No comments: