Wednesday, July 31, 2013

VIJANA WAASWA KUJITAMBUA NA KUTHUBUTU ILI KUJILETEA MAENDELEO

Waziri wa Habari Vijana,Utamaduni na Michezo Mheshimiwa Dk Fenella Mukangara akizungumza na washiriki wa kambi ya vijana leo jijini Dar es Salaam alipokuwa akifungua rasmi kambi hiyo ambayo imeanza tarehe 29 na inatarajiwa kumalizika tarehe 2 Agosti.Kambi hiyo ya vijana ya Dunia imeandaliwa na taasisi isiyo ya Kiserikali International Youth Fellowship(IYF) kwa kushirikiana na Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo.
Baadhi ya washiriki wa kambi ya vijana wakisikiliza hotuba ya Mheshimiwa Waziri Fenella Mukangara hayupo pichani alipokuwa akifungua rasmi kambi hiyo leo jijini Dar es Salaam.
Kikundi cha sanaa kutoka IYF wakicheza muziki wa kitamaduni kutoka Korea mbele ya mgeni rasmi Waziri wa Habari Vijana,Utamaduni na Michezo Mheshimiwa Dk Fenella Mukangara wakati wa hafla ya ufunguzi kambi ya vijana leo jijini Dar es Salaam.
Waimbaji wa Kwaya ya kimataifa kutoka Korea Gracias wakiimba wakati wa hafla ya ufunguzi wa kambi ya vijana l;eo jijini Dar es Salaam.
Kikundi cha sanaa kutoka Tanzania wakionyesha mchezo wa Tai Kondo leo jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Habari Vijana,Utamaduni na Michezo Mheshimiwa Dk Fenella Mukangara akiteta jambo na Mkurugenzi wa IYF Tanzania Pastor Joen Hee Yong (katika) kushoto ni mwanzilishi wa IYF Duniani Pastor Park Ock Soo.
Waziri wa Habari Vijana,Utamaduni na Michezo Mheshimiwa Dk Fenella Mukangara akifurahia kwaya ya Gracias ilipokuwa inaimba wimbo wa Taifa wa Tanzania kulia ni Mkurugenzi wa Maendeleo ya Vijana Tanzania Profesa Elisante Ole Gabriel. PICHA ZOTE NA Frank Shija - Maelezo

No comments: